Jumamosi, 25 Mei 2019

Je, Samatta kucheza Klabu Bingwa Ulaya na Genk ama kutimkia England msimu ujao?

Samatta, maarufu kama Samagoal, amedokeza kuwa kuna vilabu sita vya Ligi ya Primia ambavyo vinapigana vikumbo kumsajili.
"Kwa sasa sipo katika nafasi nzuri ya kuelezea ni klabu gani lakini pia kuna klabu nyingine mbili kutoka Hispania ambazo zimekuwa zikiisaka saini yangu. Hata hivyo, mimi ndoto zangu ni kucheza katika Ligi Kuu ya England," Samatta ameliambia gazeti la Mwananchi.
Hii si mara ya kwanza kwa Samatta kuhusishwa na uhamisho wa kwenda Ligi ya Primia, lakini inaonekana kuwa safari hii mambo yameiva.
"Ndiyo, nitaondoka mwishoni mwa msimu huu...(klabu ya England) moja inanifukuzia sana na imekuwa ikipiga simu kwa wakala wangu kila siku," amesema Samatta.
Samatta

Katika dirisha dogo la usajili la mwezi Januari mwaka huu, klabu ya Cardiff ilituma ofa ya Pauni milioni 13 kumng'oa Genk, lakini uhamisho huo ukakwama.
Klabu ya hata hivyo Cardiff imeshuka daraja.

Ukiachana na Cardiff, vyombo vya habari vya Uingereza mwaka jana viliripoti klabu nyengine tatu za nchini humo amabazo zilikuwa zikihusishwa na kutaka huduma ya ushambuliaji kutoka kwa Samatta.
Klabu hizo ni Everton, WestHam na Burnley.

Samatta ameendelea kuwa kipenzi cha mashabiki wa Genk msimu huu baada ya kuongoza safu ya ushambulizi wa timu hiyo na kunyakuwa ubingwa wa ligi hiyo baada ya kuukosa kwa miaka nane.
Streka huyo mwenye miaka 26, ameifungia Genk magoli 23 na kumaliza kama mshambuliaji bora wa ligi. Pia ameifunga magoli 9 kwenye michuano ya ligi ya Europa.

Jina la Samatta limekuwa likiimbwa na mashabiki wa Genk, na wamekuwa wakimuomba mshambuliaji huyo kusalia klabuni hapo kucheza ligi ya Mabingwa Ulaya. Samatta ameiambia Mwananchi kuwa moyo wake upo England japo kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Ligi ya Mabingwa ni kitu cha kutamanisha pia.
Jina la Samatta limekuwa likiimbwa na mashabiki wa Genk, na wamekuwa wakimuomba mshambuliaji huyo kusalia klabuni hapo kucheza ligi ya Mabingwa Ulaya. Samatta ameiambia Mwananchi kuwa moyo wake upo England japo kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Ligi ya Mabingwa ni kitu cha kutamanisha pia.
Samatta


Hata akihamia England, bado atakuwa ameweka rekodi ya kuwa mtanzania wa kwanza kufanya hivyo. Pia amekuwa Mtanzzania wa kwanza kucheza Ligi ya Europa.

"Hawa jamaa (Genk) hawajacheza Ligi ya Mabingwa tangu mwaka 2011 enzi za akina (Kevin) De Bruyne, najua wanataka nicheze msimu ujao lakini Ligi Kuu ya England ina heshima yake...ni ligi ambayo tayari imepiga hatua kubwa sana kulinganisha na Ligi Kuu ya Ubelgiji. Ni ligi ambayo inapendwa na watu wengi duniani, Ligi inayoonekana sehemu kubwa duniani. Yaani kwa vitu vingi iko mbali."
Samatta alijiunga na Genk akitokea TP Mazembe Januari 2016 ambapo alitia saini mkataba wa kumuweka katika klabu hiyo hadi msimu wa 2019/20.
Amesalia na miezi 12 kabla ya mkataba wake kumalizika.
Samatta alihamia Ubelgiji mwaka mmoja baada ya kutawazwa mchezaji bora wa mwaka Mwafrika aliyekuwa anacheza ligi za barani Afrika mwaka 2015.
Alishinda vikombe sita vikuu akiwa na TP Mazembe ikiwa ni pamoja na kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2015 kabla ya kuondoka.
Alishinda vikombe sita vikuu akiwa na TP Mazembe ikiwa ni pamoja na kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2015 kabla ya kuondoka.

    Ijumaa, 10 Mei 2019

    Tanzania yataka wananchi kutoizingatia ripoti ya IMF iliyovuja na kuonesha kasi ya uchumi wa nchi hiyo imeshuka

    Sarafu ya Tanzania
    Serikali ya Tanzania imewataka raia wake kuipuuzia ripoti iliyovuja ya ukuaji wa uchumi wa nchi hiyo iliyoandaliwa na Shirika la Fedha Duniani (IMF).
    Waziri wa Fedha wa Tanzania, Dkt Philip Mpango ametoa rai hiyo Bungeni hii leo alipokuwa akijibu hoja za upande wa upinzani kuhusu ukuaji wa uchumi.
    "Hii niliyoshika ni ripoti ya IMF. Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) inakadiria uchumi wa Tanzania atakuwa kwa asilimia 6.8 na Benki ya Dunia inakadiria uchumi wetu utakua kwa asilimia 6.6 mwaka 2019. Hiyo taarifa unayoitumia ni ile iliyovuja."
    Gazeti la Mwananchi limemnukuu Mpango akisema hayo alipokuwa anampa taarifa mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde aliyeinukuu ikionyesha uchumi wa Tanzania unakua kwa wastani wa asilimia nne.
    Ripoti iliyovoja ya IMF inakadiria kuwa uchumi wa Tanzania utakua kwa asilimia 4.4 mwaka 2019 toka asilimia 6.6 kwa mwaka uliopita.
    Sakata la ripoti hiyo lilianza katikati ya mwezi Aprili ambapo IMF kupitia tovuti yake ilitoa taarifa kuwa imenyimwa ridhaa na Tanzania kuchapisha ripoti baada ya wataalamu wake kukamilisha tathmini yao nchini humo.
    Matokeo ya ripoti hiyo hata hivyo yalivuja muda mfupi baadae na kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa kama Reuters na Bloomberg.
    Jambo hilo lilizua gumzo kubwa ndani na nje ya Tanzania huku wapinzania wakiitaka serikali ya nchi hiyo kuvunja ukimya
    Wiki moja baadae, Mpango alitoa ufafanuzi na kueleza kuwa serikali ya Tanzania haijazuia kuchapishwa kwa ripoti hiyo bali inaendelea na mazungumzo na IMF.
    Mpango alidai kuwa kuna hoja za upande wa Tanzania ambazo hazikutiliwa maanani na wataalamu wa IMF.
    Hata hivyo maelezo ya waziri huyo bado yaliendelea kukosolewa. Mtaalamu wa uchumi na kiongozi wa chama cha upinzani CUF Prof Ibrahim Lipumba aliiambia BBC Swahili kuwa, kwa utaratibu, mpaka inapofikia hatua ya kuchapishwa, majadiliano yanakuwa yameshafungwa.
    "Kimsingi hakuna tena majadiliano, serikali yetu itoe tu ridhaa ili ripoti ichapishwe," alisema Lipumba.

    Utaratibu wa IMF kuchapisha ripoti

    Dar es Salaam
    Image captionTanzania ni ya pili kwa uchumi mkubwa Afrika Mashariki nyuma ya Kenya
    Kupitia kifungu cha nne cha makubaliano, IMF inaruhusiwa kuchunguza uchumi , hali ya kifedha na sera ya ubadilishanaji wa fedha ya wanachama wake ili kuhakikisha kuwa mfumo wake wa kifedha unatekelezwa bila matatizo yoyote.
    Hatua hiyo inashirikisha ziara ya maafisa wa IMF ya kila mwaka katika taifa hilo ili kuangazia data mbali na kufanya vikao na serikali pamoja na maafisa wa benki kuu.
    Baadaye wanatoa ripoti kwa bodi kuu, ambayo hutoa maoni yake kwa serikali na kuchapisha ripoti hiyo katika tovuti yake baada ya kupata ruhusa kutoka kwa taifa hilo

    Ryan Muiruri: Kijana aliyezaliwa na jinsia mbili nchini Kenya

    Ryan MuiruriHaki miliki ya pichaRYAN MUIRURI
    Image caption'Mimi sikujua kwamba niko tofauti na watoto wengine wakike, niligudua hilo nilipokuwa na umri wa miaka mitano' Ryan Muiruri
    Hujafa hujaumbika, miaka 29 iliyopita kijana aliyezaliwa na jinsia mbili nchini Kenya Ruth Wangui amebadili jinsia yake na sasa ni mwanamume anayefahamika kama Ryan Muiruri.
    Ni mojawapo ya watoto wengi wanaozaliwa duniani kila mwaka walio na umbo lisiloweza kufafanuliwa kuwa ni mwanamke au mwanamume kwa wakati huo.
    Kulingana na Ryan, alipozaliwa, mamake na mkunga waliamua kumpatia jinsia ya kike kwani walimuona kuwa na maumbile ya mtoto msichana.
    Uamuzi ambao haukumpatia amani katika miaka itakayofuata
    Baadhi ya watu wanaozaliwa na jinsia mbili, wanataka kutofautishwa na wapenzi wa jinsia moja, kwani hali zao wanaeleza ni kuhusu jinsia wala sio sifa za uume au uke.
    Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, kuna aina 42 tofauti ya watu wenye jinsia mbili ulimwenguni. Ijapokuwa hakuna takwimu zilizokusanywa kuhusu hili, wataalamu wanasema kuwa, kwa kila watoto elfu 20 wanaozaliwa, mmoja ana jinsia mbili.
    'Mimi sikujua kwamba niko tofauti na watoto wengine wakike, niligundua hilo nilipokuwa na umri wa miaka mitano nilipokuwa nikicheza na wenzangu' Ryan amesema.
    'Nilikuwa nikicheza wa wenzangu na shangazi yangu ambaye tuko rika moja, na baada ya muda nilianza kupigana na mwenzangu hapo ndipo wakagundua kwamba mimi sio mtoto msichana kamili kama walivyodhania, walinivua nguo na hapo ndipo niliweza kubaini kwamba ni kweli mimi niko tofauti, niligundua niko na sehemu nyengine ambazo wasichana wengine hawana.' Ryan aliongezea.
    Anaeleza kwamba watu wenye jinsia mbili hubaguliwa, wengi hukosa kueleweka, na mara nyingi hutizamwa kama watu wenye laana.
    Ryan Muiruri
    Walinivua nguo na hapo ndipo niliweza kubaini kwamba kweli, mimi niko tofauti. Niligundua nina sehemu nyengine ambazo wasichana wengine hawana.'
    Ryan Muiruri
    Ryan ambaye sasa ni mwanaharakati na muasisi wa chama cha watu wenye jinsia mbili, anasema hali hii ya kuwa na jinsia mbili iliathiri maisha yake.
    'Nilikuwa sina raha na hata marafiki zangu walinifanyia utani wakisema mimi huwa sitabasamu, lakini ni kwa sababu sijakutana na kitu chochote ambacho kimenifurahisha maishani mwangu.'
    'Tangu kisa hicho cha watoto kugundua kwamba mimi sio msichana kamili walienda shuleni na kutangaza siri yangu. Wakati nilipokuwa ninakwenda haja watoto walikuwa wakinifuata kunitazama iwapo mimi hujisaidia kama kijana au huchuchumaa kama msichana, na maisha shuleni yalizidi kuwa magumu sana kwangu'.
    Anaeleza hayo yalimfanya kutoroka shuleni na hata kujificha msituni lakini baada ya muda hilo likagunduliwa.
    'Mamangu mzazi aligundua hilo kwani sikuwa na andika chochote katika vitabu vyangu'.
    Mwaka wa 2004, ndipo aliianza safari ya kubadili jinsia yake kuwa mwanamume na anasema ulikuwa mwaka mgumu sana.
    'Mahali nilipolelewa walizingatia dini sana, kwa sababu hata watoto wasichana hawakuruhusiwa kuvaa suruale ndefu ila marinda pekee'.
    'Nilipopata muda wa kutoka nyumbani nilikuwa najifanya kijana na nikaanza kuvalia mavazi ya kakangu mdogo lakini niliporudi nyumbani ilinibidi nivae rinda na kujifanya mimi mi msichana kwani hivyo ndivyo wanavyonitambua
    Ryan anakiri kwamba ni mtihani mkubwa na amewasihi wazazi iwapo watagundua kwamba wamejaliwa mtoto wenye utata au tofauti kidogo, ni vyema kutafuta ushauri kwa wakati muafaka na hata amewasihi wale ambao wana jinsia mbili kujitokeza watafute uhuru wa maisha yao.
    Sheria Itakayowasimamia watu wenye jinsia mbili yawasilishwa kwa mwanasheria mkuu Kenya

    Mtoto anazaliwa vipi na jinsia mbili?

    Kulingana na Dkt. Andrew Remideus kutoka nchini Tanzania, hali hiyo hutokea katika utungishi wa mimba katika wiki ya tano au sita, ambapo kunatengenezwa jinsia kati ya kike na ya kiume na ndio hitalafu hutokea.
    Na hitalafu hiyo husababisha utata wa kubaini jinsia kamili.

    Kabla ya kufanya upasuaji wa kubadilisha mtu jinsia lazima daktari azingatie yafuatayo

    •Mtu kufanyiwa vipimo
    •Kubainisha viungo alivyonavyo vya uzazi
    •Idadi ya homoni katika mwili wake
    •hali ya mtu huyo anajihisi.
    Hata hivyo, katika kipindi cha miaka michache iliyopita, watoto wenye jinsia mbili wamefanyiwa upasuaji na kuwa sawa. Upasuaji ambao hufanywa mara nyingi hurekebisha tu sehemu zenye matatizo kwa sababu sio lazima. Baadhi ya watu waliofanyiwa wanasema kuwa upasuaji huo ulikuwa na athari hasi maishani mwa watoto, kimwili na pia kiakili.
    Ili kuwalinda watoto dhidi ya ukiukwaji huu, mataifa kama vile Malta, Ujerumani, Chile, Indonesia na Colombia yamepiga marufuku upasuaji wa aina hiyo kwa kuwa unafanywa bila ya kuzingatia maslahi ya mtoto.
    Nchini kenya mchakato huo umeanza na jopokazi lililobuniwa na serikali ya Kenya kuchunguza sera na sheria zilizopo kuhusu watu wenye maumbile hayo, wamependekeza watambuliwe kama "jinsia ya tatu".
    Jopo hilo pia linapendekeza jinsia ya watu hao ijumuishwe katika stakabadhi rasmi na vile vile washirikishwe katika sensa ya kuhesabu watu.
    Ujerumani, ni taifa la kwanza duniani kuanzisha jinsia ya tatu kwa kuruhusu watoto wanaozaliwa na jinsia tatu kusajiliwa kuwa si wanaume au wanawake

    Mdude Chadema: Mwanasiasa wa Tanzania asimulia kisa cha utekaji wake na mateso aliyopitia


    Mwanaharakati wa Tanzania Mdude NyagaliHaki miliki ya pichaMDUDE NYAGALI/ FACEBOOK

    Mwanaharakati wa chama cha upinzani nchini Tanzania Mdude Nyagali ameelezea matuko yaliopelekea hadi kutekwa kwake kwa siku tatu kabla ya kujipata porini katika eneo la Mbeya.
    Mdude ambaye aliokolewa na wanakijiji ambao walimpeleka katika hospitali ya eneo hilo alipatikana akiwa mchovu na aliyeteswa wakati wa kipindi chote cha utekaji wake.
    Akizungumza na runinga ya ROYMEDIA HOUSE nchini Tanzania katika kitanda chake hospitalini ambapo amelazwa, mwanaharakati huyo alisumilia kwamba watu waliomteka waliwasili na gari moja siku ya Jumamosi jioni nje ya makaazi yake.
    Polisi wanachunguza tukio hilo na wamekanusha madai ya kuhusika na kutekwa kwakeMwanaharakati wa Tanzania Mdude Nyagali


    Kulingana na mwanaharakati huyo ambaye wakati wote huo alikuwa akiwaangalia watu hao kupitia dirisha la kibanda, cha kushangaza ni kwamba waliokua ndani ya gari hilo walisalia ndani bila kutoka.
    ''Ilipofika kati ya saa kumi na moja na kumi na mbili jioni watu hao walikuja hadi pale nilipokuwa na kuanza kuomba vocha ya simu wakati mimi nilikuwa katika mtandao ndani ya simu yangu. Nikawaambia sina akarudi ndani ya gari alilokuwemo''.
    Mwanaharakati huyo anaelezea kwamba alianza kuwa na wasiwasi akaamua kurudi nyumbani kwake.
    Anasema kwamba wakati huo alikuwa amebaba stakabadhi muhimu, ikiwemo simu na laptopu yake.
    Anaongezea kwamba alipokuwa akielekea nyumbani kwake watu watatu walitoka ndani ya lile gari na kumfuata hadi karibu na mlango wa nyumba yake.
    Anasema kwamba mmoja ya watu hao alisimama upande wake wa kushoto mwengine upande wa kulia na watatu akasimama katikati.
    ''Mimi niliegemea ukuta mmoja akaniambia ndugu sisi ni askari tunahitaji kuondoka nawe, nikawauliza wajitambulishe'', alisema
    Lakini jamaa hao watatu walianza kumkaribia na alivyoona vitendo vyao akaanza kurudi nyuma akijaribu kutoroka lakini mmoja akamwambia mwenzake aliyekuwa karibu naye ''kamata begi na simu ndio vitu muhimu''
    Mwanaharakati huyo ambaye alionekana kuwa na maumivi akisumilia kisa hicho anasema kuwa alijaribu kutoroka na begi hilo lakini mmoja ya watekaji hao alilikamata begi lake na kuanza kuvutana nalo
    Nilivuta begi langu nikaona hataki kuachilia nami nikaanza kupiga kelele ili watu wakusanyike mahala nilipokuwa kwa sababu tayari giza lilikuwa limeanza kuingia''.
    Anasema aliimarisha kelele zake kwa kuwa eneo analoishi ni karibu na kituo kimoja cha polisi na mita kumi kutoka kwa benki.
    Anasema kwamba alipokuwa akipiga kelele za usaidizi jamaa hao walijaribu kumfunika mdomo na kufanikiwa kumnyang'anya begi lake lililokuwa na laptopu.
    Walimburuta wakimuelekeza katika gari lao na watu walipojaribu kutaka kuingilia na kumsaidia mmoja wa watekaji hao anadaiwa kutoa bunduki na kuwatishia.
    ''Waliwatishia watu waliokuwa wamewasili kwa bunduki wakarudi nyuma, nami nilipoona vile nikaona hapa sasa ni kutetea nafsi yangu na nikaanza kupambana nao'', alisema Mdude.
    Hatahivyo kulingana na mwanachama huyo wa chama cha upinzani nchini Tanzania Chadema, watu hao walimshinda nguvu na kumuingiza katika gari lao na kuondoka naye.
    Awali baada ya taarifa za kutekwa Mdude kusambaa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, George Kyando alikanusha katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi nchini Tanzania kusikika kwa milio ya risasi, siku iliotajwa.
    "Mimi ni mkazi wa eneo linalodaiwa kuwa risasi zimepigwa lakini sijasikia na kama unavyojua mji wa Vwawa ni mdogo ambao zikipigwa risasi lazima utasikia," alisema.
    Kamanda Kyando aliahidi kwamba ataendelea kufuatilia kwa kina taarifa hizo.
    ''Nikiwa ndani ya gari lile nilipigwa sana kwa kutumia chupa , walivua viatu nilivyokuwa nimevaa wakanipiga navyo usoni na masikioni na baadaye kunifunga kamba usoni na mdomoni na nikapoteza fahamu'', aliongezea Mdude.
    Anasema kwamba alipopata fahamu alijipata katika msitu akiwa hajui aliko
    Anaongezea kwamba alijaribu kutoa kamba ambazo alikuwa amefungwa mdomoni na kuanza kutafuta usaidizi
    ''Niliinuka nikaanza kutembea pole pole nikitafuta usaidizi hadi nikafika barabarani, nikiwa barabarani nilijaribu kusimamisha magari yaliokuwa yakipita lakini hayakusimama kwa zaidi ya saa moja hadi msamaria mwema mmoja aliposimama na kuwaita watu wa eneo la kijiji ili wanisaidie'', alisema
    ''Maneno niliyokuwa nikiyasikia masikioni mwangu ni mpige hivi mpige vile'', aliongezea .
    Anasema kwamba kutekwa kwake kunahusiana na maswala ya kisiasa na ndio maana watekaji wake walichukua simu yake na laptopu.
    ''Simu na laptopu yangu zilikuwa na vitu muhimu sana , maswala ya chama, mambo ya kesi na mafunzo'', alisema
    Hatahivyo mwanasiasa huyo amesisitiza kuwa hatosita kupigania haki za raia mbali na kuisahihisha serikali inapokosa na kuipongeza inapofanya vyema.
    ''Nitasimamia kupigania haki za watu , siwezi kunyamazia makosa. Tukiamua sote tuwe upande mmoja, viongozi wa chama tawala watakuwa na kazi gani?', aliuliza.
    ''Wana kazi kwa sababu kuna upinzani wakinipoteza mimi na wengine wengine watajitokeza na kuendelea'', alimaliza