Jumapili, 5 Mei 2019

The Week in Books New titles to watch for in May, a Canadian bookstore chain heads to the U.S. and more




We take the weekend to highlight recent books coverage of note in The Times:
Julie Orringer’s new novel, “Flight Portfolio,” is, according to the critic and author Cynthia Ozick, a “prodigiously ambitious” one. It is historical fiction and a kind of fictionalized biography, the study of the real-life World War II figure Varian Fry. It is also a Holocaust novel and a tale of suspense. There’s a lot to dig into, and Ozick does just that with characteristic insight and flair. One of our greatest living critics, Ozick last wrote for the Book Review about the role of gossip in storytelling. Zoë Heller reviewed her most recent collected work here.
We’ve also got reviews of fiction from Jennifer duBoisStewart O’Nanand Laila Lalami, who joins us on the podcast this week.
Don’t miss one nonfiction review of note from The Times’s own Paul Krugman, who reviews “Firefighting: The Financial Crisis and Its Lessons,” written by Ben Bernanke, Timothy Geithner and Henry Paulson Jr. They were all there, and in addition to turning out a primer on the crisis and a tick-tock of what happened, they offer, as Krugman puts it, “a very scary warning about the future.”
Dwight Garner reviews Ali Smith’s new novel, “Spring,” the latest in a projected seasonal cycle. Its among her more political novels, dealing with Brexit, immigration, climate change and a host of other Garner writes that it “taps deeply into our contemporary unease. It’s always alive.”
The science of mental illness has vexed researchers for generations, and the Harvard scholar Anne Harrington takes up the subject in her new book, “Mind Fixers: Psychiatry’s Troubled Search for the Biology of Mental Illness.” In her review of the book, Jen Szalai writes, “It turns out that psychiatry’s understanding of mental illness is full of hairpin turns and unintended consequences.”
In an essay last week, our critic Parul Sehgal looks at recent wave of remarkably various books, all which remind us of the kind of touchy ethical explorations the novel makes possible. As she writes, “They trouble debates that traffic in certainties; they come laden with confusion, doubt, subtlety — is it excessively earnest to call it truth?"
A new month means a new crop of books. Here’s a list of our 14 most anticipated books coming out this month, including George Packer’s latest title and a new look at Harper Lee’s life. The author of that book, Casey Cep, spoke with our reporter about her project, which delves into a true crime book that Lee never finished. “I felt like there was one thing I could do which she was never going to do, which was talk about her,” Cep said of Lee. “It’s the story behind the story. She would never have included herself.”
Separately, here are 10 books our editors recommend this week.
Indigo is expanding to the United States with its new model for how a big bookstore chain can thrive in the era of online retail.
Earlier this year, the writer Amélie Wen Zhao pulled her debut young adult novel before it was published, amid criticism that it was racially insensitive. But now, she’s changed her mind


Ni kwanini si rahisi kumpata mtu kama Mengi nchini Tanzania?

Imekuwa ni wiki ya majonzi kwa Watanzania na majirani zake baada ya kupokea taarifa ya kifo cha Reginald Mengi tarehe 2 Mei, 2019 kilichotokea Dubai katika Falme za Kiarabu.
Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka miaka 77. Wengi wanamkumbuka kwa kuwa mfanyabiashara mahiri na mmiliki wa kampuni ya IPP Limited na IPP Institute of Technology and Innovation. Huku Watanzania wakijianda kumpumzisha, baadhi wanajiuliza iwapo Tanzania itampata mtu atakayeweza kuziba pengo aliloliacha.
Lakini Mengi alikuwa ni mtu wa aina gani?


Reginald Mengi ametajwa na wengi kuwa alikuwa ni mtu aliyetafuta maslahi si yake tu bali kwa jamii nzima ya Watanzania



Mengi amekuwa akijitoa katika kusaidia wasionacho na wenye uhitaji kwenye jamii ikiwemo walemavu wa ngozi na kugharamia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo nchini India. Kila mwaka Dr. Reginald Mengi alijiwekea utaratibu wa mwaka mpya unapoingia alikuwa akiandaa chakula cha mchana na kula na wenye ulemavu wa kila aina nchini Tanzania, kitu ambacho hakitasahaulika miongoni mwa Watanzania:
Ukarimu kwa watu wenye ulemavu ni miongoni mwa sifa zinazoendelea kuenziwa kwa Dr.Mengi
Japo alikuwa ni mwanachama wa chama tawala cha CCM Bwana Mengi aliweza kuwa na maelewano mazuri na watu wa tabaka mbali mbali wakiwemo wanasiasa wa kada mbali mbali na hivyo kuvuka mipaka ya uhasama wa kisiasa baina ya kambi mbali mbali za kisiasa nchini Tanzania.
Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Zitto kabwe anaamini bwana Regnald Mengi alikuwa na mchango mkubwa katika kukuza demokrasia nchini Tanzania
Image captionKiongozi wa upinzani nchini Tanzania Zitto kabwe anaamini bwana Regnald Mengi alikuwa na mchango mkubwa katika kukuza demokrasia nchini Tanzania
''Mengi kama alivyosema yeye alikuwa mwanachama wa CCM , lakini kusema ukweli ni mtu ambaye amekuwa akiunga mkono pia upinzani ili kuwe na upinzani imara nchini, amewahi kutoa msaada wa kufanya juhudi halali kabisa za kisasa kwa upinzani. Ni mtu ambaye alipoona kuna jambo halali la kushughulikiwa kwa ajili ya manufaa nchini alikuwa anazungumza moja kw amoja na wa pande zote kuhakikisha jambo hilo linatendeka, alikuwa na mchango mkubwa kabisa katika kuhakikisha kunakuwa na demokrasia nchini''. Ameiambia BBC, kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Zitto Kabwe.
Si Tanzania pekee alikofahamika na kupendwa na watu mbali mbali waliotambua kazi zake na mchango wake katika maendeleo ya nchi yake na maisha ya Watanzania kwa ujumla.
Hii imedhihirika baada ya kifo chake kwani watu kutoka mataifa na tabaka mbali mbali wamemwagia sifa kwenye mitandao ya kijamii hususan kupitia Twitter kupitia Hastag Mengi ilianzishwa:
Mengi hakuwa mtu wakukata tamaa
Waliomfahamu Bwana Reginald Mengi wakati wa uhai wake wanasema hakuwa mtu mwenye kukata tamaa.
Wakati mambo yalipaoonekana kwa wengine kuwa ni magumu, alitumia fursa hiyo kujitafutia suluhu ya kibinafsi na pia kutoa suluhu kwa matatizo ya jamii nzima ya Watanzania.
Mfano Mwaka wakati Tanzania ilipokumbwa na uhaba wa bidhaa karibu zote baina ya miaka ya 1983 1984, alihangaika kupata kalamu ya kuandikia na hatimae akaweza kuandika kitabu alichokiita - I Can, I Must, I Will- kinachomaanisha -Ninaweza, Lazima , nitaweza.
Bwana Mengi aliamsha ari yake ya ujasiriamali na akaamua kuanza kuagiza bidhaa kutoka nchi jirani ya Kenya.
Miongoni mwa bidhaa za kwanza alizoziagiza Mengi ni Kalamu za wino kutoka Mombasa Kenya.
"Wakati mizigo ulipowasili sikujua niiuweke wapi. Kwa hiyo , mahala pasuri pa kuiweka palikuw ani chumbani kwanguna ilikuwa ni katika chumba kileambako nilianza kupanga kalamu zangu ," aliliambia jarida la Forbes Africa toleo la Julai 2014.
Alinyimwa mkopo wa $4,000 kutoka kwa benki ya taifa ya biashara (NBC) inayomilikiwana , lakini hakukata tamaa na akaamua kuzungumza na wafanyabiashara wenzake nchini Kenya na baadaye akapata fedha hizo.
Wakati serikali ilipokabiliana na kuwakamata wafanyabiashara ikiwashutumua kwa kuuza bidhaa muhimu kiholela, ndipo Bwana Mengi alipoamua kutoacha biashara daima na kuamua kuzipanua biashara zake katika maeneo mengine, ikiwawemo kuanzisha kiwanda cha vinywaji vya Coca-Cola mjini Moshi, kilichoitwa Bonite Bottlers Mwaka 1987.
Aliuza dawa za kusafisha viatu zilizotengenezwa kwa mkaa na mafuta, na vipodozi vya kusugua mwili mwili asilia vitokanavyo na matope ya baharini
Aliendelea kutengeneza kila kitu alichokiweza kuanzia: karatasi za usafi wa maliwato, sabuni, kemikali za usafi, vitanda nadawa za meno.

Image captionSalim Kikeke mwandishi wa BBC, alimfahamu Bwana mengi kama mtu ambaye hakujikweza japo alikuwa na umaarufu na utajiri mkubwa
Na hatimae akaamua kujitosa katika uwekezaji katika tasnia ya habari na kumiliki vyombo mbali mbali vya habari yakiwemo magazeti, redio na televisheni ambavyo vilimpatia umaarufu mkubwa.
Licha ya mazingira magumu ya uhuru wa habari nchini Tanzania, Mengi aliweza kujitosa katika tasnia ya habari na kuanzisha vituo mbali mbali vya televisheni, redio na magazeti ambavyo vimetoa mchango mkubwa wa ajira na kukuza vipaji vya kwa waandishi wa habari nchini Tanzania.
''Kwa kweli naweza kusema hapa nilipofika sasa ni kutokana na mengi, nimepitia mikononi mwake nilipokuwa nafanya kazi katika kituo chake cha televisheni cha ITV, na hata nilipokuja huku Uingereza aliniruhusu na baadaye aliniuliza iwapo nitarudi kufanya kazi Tanzania kufanya kazi ITV, nikamwambia bado ninafanya kazi hapa, lakini akashauri kuwa iwapo ningependa kuendelea kufanya kazi BBC ni sawa tu niendelee. Kwa kawaida si waajiri wengi watakaokuambia uendelee kufanya kazi ulipo huku wakiona una kipaji na unawaponyoka'' Alisema mwandishi wa Televisheni ya Kiswahili ya BBC - Swahili Dira TV, Salim kikeke alipokuwa akimkumbuka Bwana Mengi.
Salim aliongeza kuwa: '' Kitu kingine nilichojifunza kwake ni kwamba japo alikuwa ni mtu tajiri mwenye mafanikio na umaarufu lakini hakujikweza alikuwa ni mtu wa watu, hilo nimejifunza kutoka kwake''
Hadi mauti yake Bwana Mengi alikuwa muanzilishi na mwenyekiti mtendaji wa IPP Limited pamoja na IPP Institute of Technology and Innovation


Tetesi za Soka Ulaya Jumapili 05.05.2019: Lacazette, Pogba De Gea, Navas, De Ligt, Hazard

Golikipa wa kimataifa raia wa Uhispania David de Gea, 28, amepewa wiki moja ili kuamua mustakabali wake na klabu yake ya Manchester United. (Sun)
Barcelona wametangaza dau nono na la kushtukiza la pauni milioni 70 ili kumnasa mshambuliaji wa Arsenal Mfaransa Alexandre Lacazette, 27. (Sunday Express)
Manchester United wanaweza wakapewa nafasi ya kumsajili kipa wa Real Madrid Keylor Navas, 32, katika kipindi hiki ambacho hawana uhakika endapo De Gea atasalia klabuni hapo. (Telegraph)

Chelsea wametakiwa kuheshimu makubaliano waliyoingia na na mshambuliaji wao Eden Hazard ya kuwa ili ajiunge na Real Madrid, alitakiwa kusalia klabuni hapo msimu huu na pale utakapoisha ataruhusiwa kujiunga na miamba hiyo ya Uhispania. (Sun)
Manchester City wanajipanga kuchuana na Barcelona katika mbio za kumsajili beki na nahodha kinda wa Ajax Matthijs de Ligt, 19, mwenye thamani ya pauni milioni 65. (Star)David De Gea

Matthijs de Ligt
Image captionMatthijs de Ligt
Kiungo wa Manchester United Juan Mata yawezekana akarejea Uhispania msimu ujao - huku klabu ya Athletic Bilbao ikimuwania kiungo huyo mwenye miaka 31 kwa udi na uvmba. (Mirror)
Zinedine Zidane amekataa kuhusishwa na uvumi juu ya uhamisho wa wa kiungo wa Manchester United Paul Pogba, 26, kwenda Real Madrid. (Manchester Evening News)
Paul Pogba
Image captionPogba kuihama Man United? Jibu litapatikana siku chache zijazo dirisha la usajili likifunguliwa.
Pogba ameambiwa kuwa hatapata nafasi nyengine tena ya kuhamia Madrid endapo hatafanya hivyo mwishoni mwa msimu huu. (Sun)
Beki wa Atlanta United Florentin Pogba, 28, ambaye ni kaka wa Paul, anaamin: "kuna kitu kitatokea majira haya ya kiangazi" na amekataa kusema iwapo mdogo wake hatohamia moja wapo ya klabu kubwa za Uhispania Real Madrid ama Barcelona for his sibling. (AS, via Calciomercato)
Mourinho
Image captionMourinho alitimuliwa kazi na Machester United mwezi Disemba
Kocha aliyetimuliwa kazi na Manchester United Jose Mourinho, 56, amepatiwa ofa ya kuifundisha klabu ya AS Roma kwa miaka mitatu, lakini atajiunga na klabu hiyu endapo watafuzu kushiriki michuano ya Klabu Bingwa Ulaya. (L'Equipe, via Mail on Sunday)
Kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino ameahidiwa na uongozi wa klabu hiyo kuwa atawezeshwa ili afanye usajili mkubwa hivi karibuni. (Sun)

Tetesi kali za Jumamaosi

Barcelona inaanda dau la £30m kwa Chelsea kumnunua mshambuliaji wa Chelsea na Brazil Willian, 30. (Sun)
Willian
Image captionWillian
Manchester City imefanya mkutano na wazazi wa beki wa Benfica joao Felix 19 ambaye amehusishwa na uhamisho wa kuelekea Manchester United na Liverpool. (Record, via Express)
Mkufunzi wa klabu ya Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameanzisha harakati zake za kumsajili mshambuliaji wa Lyon Moussa Dembele, 22. (L'Equipe, via Mirror)
Ole Gunnar Solskjaer
Image captionOle Gunnar Solskjaer
Chelsea itaanzisha mazungumzo na kiungo wa kati wa Uingereza Ruben Loftus-Cheek, 23, kuhusu mkataba mpya . (Sun)
Mshambuliaji wa Colombia James Rodriguez, ambaye yupo kwa mkopo katika klabu ya Bayern Munich, atauzwa kwa dau la £36m na Real Madrid mwisho wa msimu huu na klabu za Manchester United na Chelsea huenda zina hamu ya kumsajili mchezaji huyo.27. (Marca, via Express)
James Rodriguez
Image captionJames Rodriguez
Mchezaji wa Paris St-Germain aliyesainiwa kwa rekodi ya dunia Neymar, 27, huenda akauzwa kwa dau la £145m mwisho wa msimu huu kutokana na sheria inayomzuia kuuzwa . (Mundo Deportivo, via Mirror)
Mkufunzi wa Tottenham Mauuricio Pochettino ameonya Tottenham kwamba atalazimika kufanya mabadiliko yenye 'uchungu' mkubwa ili kuimarisha klabu hiyo kuwa katika kiwango cha uwanja mpya. (London Evening Standard)


"Vilio vya kudhurumiwa ardhi ni vingi, kuliko kuhesabu Makaburi" Steve N...




Tunayo stori kutokea kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Wazalendo Kwanza, Steve Nyerereambapo amewaongoza wasanii kuingia mikataba ya kupewa viwanja maeneo ya Kigamboni, Dar es Salaam.
Steve Nyerere ambaye pia ni msanii wa maigizo, amefunguka na kusema kuwa waliahidiwa na taasisi mbalimbali kupatiwa viwanja lakini mwisho wa siku hawapati, hali ambayo imekuwa ikiibua vilio kwa wasanii


Steinunn Gunnsteinsdóttir: Mwanzilishi wa kampuni ya utengenezaji ngozi ya samaki

Steinunn Gunnsteinsdóttir anakiri kuwa iliichukua familia majaribio ya mara kadhaa kuweza kutengeneza ngozi kutokana na samaki.
"Mara 200 ya kwanza tulitengeneza supu ya samaki iliyokuwa na harufu kali," alisema.
Bi Gunnsteinsdóttir ni meneja wa mauzo wa kampuni ya Atlantic Leather kutoka Iceland ambayo inajihusisha na biashara ya bidhaa za samaki Barani Ulaya
Tangu mwaka 1994 kampuni hiyo imekuwa ikitengeneza ngozi kutokana na samaki wa aina kadhaa kama vile salmon, perch, na cod.
Shughuli ya kutengeneza ngozi hiyo huchukua kati ya wiki mbili hadi tatu, na wafanyikazi 19 wanaweza kutengeneza karibu tani moja ya ngozi ya samaki kwa mwezi.
"Harufu ya samaki hubadilika katika awamu ya kwanza ya utengenezaji wake, na baadaye hubadilika na kunukia kama ngozi ya kawaida," anaongeza Bi Gunnsteinsdóttir.
Ngozi ya samaki inaendelea kupata umarufu wa kutengenezewa vibeti vya wanawakeHaki miliki ya pichaFAO/LUIS TATO
Image captionNgozi ya samaki inaendelea kupata umarufu wa kutengenezewa vibeti vya wanawake
Kampuni hiyo inapata malighafi yake kutoka Iceland, Norway na visiwa vya Faroe.
Tofauti na utengenezaji wa ngozi inayotokana na ng'ombe ambayo inasemekana kuwa hatari kwa mazingira utengenezaji wa ngozi wa samaki ni salama kwa mazingira.
Atlantic Leather pia inatumia 'dye' ya kawaida na ile isiyo na athari kwa mazingira kutengeneza ngozi kutokana na samaki
Bei ya ngozi inategemea aina ya samaki kwa mfano ngozi inayotokana na samaki aina ya salmon inauzwa kwa dola $12.
Kipochi kilichotengenezwa kutokan na ngozi ya samakiHaki miliki ya pichaCAMILLE THIEBAUT
Image captionKipochi kilichotengenezwa kutokan na ngozi ya samaki
Bidhaa zao zinaagizwa sana na kampuni maarufu za mitindo kama vile Jimmy Choo, Dior na Ferragamo, na Bi Gunnsteinsdóttir anasema kumekuwa na dhana kuwa ngozi inayotokana na samaki sio dhabiti na inaweza kuchanika kwa urahisi.
"Ngozi ya samaki ni imara mara kumi zaidi ya ngozi ya ng'ombe" anasema.
"Hii ni kwasababu ngozi ya samaki inapitana pitana bada ya kwenda juu na chini... hali ambayo inaifanya kuwa thabiti zaidi hasa kwa utengenezaji wa mishipi, viatu na vibeti vya wanawake."
Japo ngozi inayotokana na samaki inachangia chini ya 1% ya mauzo ya ngozi duniani, shirika la chakula na kilimo duniani (FAO) kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa zinahamasisha ukuzaji zaidi wa ngozi hiyo ili kuwaongezea kipato wafanyibiashara wa smaki duniani.
Wafanyikazi wa kiwanda cha ngozi cha Victorian Foods nchini KenyaHaki miliki ya pichaFAO/LUIS TATO
Image captionWafanyikazi wa kiwanda cha ngozi cha Victorian Foods nchini Kenya
"Tunadhani ngozi ya samaki ndio njia bora ya kuimarisha maisha ya watu bila kuhatarisha usalama wa chakula ," anasema Jackie Alder,ambaye ni afisa wa kitengo cha uvuvi wa shirika la FAO
Ongezeko la upatikanaji wa ngozi ya samaki litapunguza uhitaji wa ngozi ya nyoka na wanyama wengine ambao wakabiliwa na hatari ya kuangamia duniani
Utumiaji wa ngozi ya samaki pia siku zijazo huenda ikapunguza uhitaji wa ngozi ya ng'ombe ambayo mfumo wake wa utengenezaji sio salama kwa mazingira.
Viwanda vya utengenezaji ngozi inayotokana na ng'ombe imehusishwa moja kwa moja na ongezeko la ulaji nyma.
Kiwango cha sasa cha ulaji nyama na ngozi ya ng'ombe kinakadiriwa kuchangia tani milioni ya uchafuzi wa mazingira kila mwaka.Tangu mwaka 2005, makundi ya kampuni zinazojihusisha na utengenezaji ngozi ambayo wanachama wake ni pamoja naAdidas, Nike na Primark -yanasema yamekuwa yakishinikiza umuhimu wa kutunza mazingira.
Mkurugenzi wa Victorian Foods James AmbaniHaki miliki ya pichaFAO/LUIS TATO
Image captionVictorian Foods inapata malighafi yake kutoka kwa wavuvi 300
Kampuni ya Kenya inayofahamika kama Victorian Foods pia kwa ushirikiano na Jackie Alder na kundi lake wanatumia samaki kutoka ziwa Turkana kutengeneza ngozi.
Afisaa mkuu mtendaji wa Victorian Foods' James Ambani anasema katika kipindi cha miaka mitatu cha utendakazi wake kampuni hiyo sasa inatengeza kilo 400 za ngozi kwa wiki ambayo inauzwa kwa dola tano kwa mraba.
Kampuni hiyo imewaajiri wanawake 10 na imekuwa ikiwapa mafunzo makundi ya watu wanaojihusisha na biashara ya utengenezaji ngozi inayotokana na samaki.
Ngozi ya samaki huenda ikapunguza uhitaji wa ngozi ya mambaHaki miliki ya pichaFAO/LUIS TATO
Image captionNgozi ya samaki huenda ikapunguza uhitaji wa ngozi ya mamba
Mwanamitindo wa mavazi mzaliwa wa Kenya Deepa Dosaja hivi karibuni alitumia ngozi ya samaki kutengeneza vibeti vya wanawake..
"Hii ni fasheni ya hali ya juu na inapendeza sana - najivunia kuimarisha taaluma yangu," anasema.