Jumapili, 3 Februari 2019

Tuna El-Gebel: Kaburi lenye miili hamsini iliohifadhiwa lapatikana Minya Misri

  Miili 50 iliokuwa imehifadhiwa na inayodaiwa kutoka katika enzi za Ptolemaic (miaka ya 305-30BC imepatikana na mwanakiolojia, kulingana na wizara ya vitu vya zamani.
Miili hiyo ambayo 12 kati yao walikuwa watoto ilipatikana katika makaburi manne yenye kina cha urefu wa mita tisa katika eneo la Tuna El-gebel huko Minya kusini mwa mji mkuu wa Cairo.
Baadhi ya miili hiyo ilikuwa imefungwa ndani ya kitambaa huku mingine ikiwa ndani ya majeneza ya mawe na yale ya mbao.  Hawajatambulika ni watu gani , maafisa wanasema lakini huenda walishikilia nyadhfa za juu.

Eeneo la Tuna El-GebelHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionEneo la Tuna El-Gebe llililopo Minya, kusini mwa mji wa Cairo
Miili iliofungwa ndani ya kitambaa ikiwa na vipande vipande vya michoro.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionVipande vipande vya mawe vilvyochorwa vilikuwa ndani ya miili hiyo.
Miongoni mwao ni fuvu hili la kichwa liliofungwa ndani ya kitambaaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMiongoni mwao ni fuvu hili la kichwa liliofungwa ndani ya kitambaa
Watoto ni miongoni mwa miii iliopatikana huko MinyaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWatoto ni miongoni mwa miii iliopatikana
Baadhi ya miili hiyo ilipatikana ndani ya majeneza ya maweHaki miliki ya pichaAFP
Image captionBaadhi ya miili hiyo ilipatikana ndani ya majeneza ya mawe
Wizara ya vitu vya zamani nchini Misri inasema kuwa miili hiyo huenda inatoka kwa watu wa familia zinazojiwezaHaki miliki ya pichaAFP
Image caption
Wizara ya vitu vya zamani nchini Misri inasema kuwa miili hiyo huenda inatoka kwa watu wa familia zinazojiweza     Egyptian mummies

Maurizio Sarri: Hazard na Higuain ni hatari sana

     Mkufunzi wa Chelsea Maurizio Sarri anasema kuwa Gonzalo Higuain na Eden Hazard ni moto wa kuotea mbali baada ya wawili hao kufunga magoli mawili kila mmoja katika mechi ya ushindi dhidi ya Huddersfield hatua ilioirejesha Chelsea katika nafasi yake ya nne.
Lilikuwa bao la kwanza la Higuain tangu alipojiunga na Chelsea kwa mkopo kutoka Juventus katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari.
''Higuian anazidi kuimarika'' , alisema Sarri.  Hakuwa katika kiwango chake cha kawaida alipowasili, kwa sababu alikuwa na jeraha la mgongo kwa hivyo akacheza kwa dakika chache''.
''Ni mchezaji mzuri. Mbali na magoli hayo ni mzuri kushirikiana karibu na Eden''.
Raia huyo wa Argentina alifunga goli la kwanza kunako dakika 16 katika mechi hiyo iliochezwa katika uwanja wa Stamford Bridge.
N'Golo Kante alimpatia pasi murua akaweza kuichenga safu ya ulinzi na kufunga. Kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika Elias Kachunga alimuangusha Cesar Azpilicueta na refa Paul Tierney akampatia penalti, licha ya fauli hiyo kuonekana kufanyika nje ya eneo hatari.
Higuain na Eden Hazard
Hazard alifunga penalti hiyo na kufunga bao lake la kwanza la ligi tangu Dusemba 26.
Raia huyo wa Ubelgiji alifanya mambo kuwa 3-0 kunako dakika ya 66, alipomzunguka kipa Jonas Lossl na kufunga kutoka pembeni.
Na dakika tatu baadaye Higuain alipata bao lake la pili baada ya kuukunja mkwaju wake karibu na lango la wapinzani .
David Luiz alifunga bao la tano katika dakika za mwisho baada ya kufunga kichwa kikali kutoka kwa kona iliomfanya Kachunga kujifunga.
Ushindi huo ulisitisha wiki mbaya ya Sarri kufuatia matokeo mabaya ya kichapo cha 4-0 dhidi ya Bournemouth.
Chelsea sasa iko nafasi ya nne , ikiwa na pointi tatu juu ya Arsenal ambao wanacheza dhidi ya Man City siku ya Jumapili.
Lakini ni kipigo cha 11 kati ya mechi 12 kwa Huddersfield ambao wanasalia chini ya jedwali la ligi .Higuain akifunga mojawapo ya magoli yake mawili dhidi ya Huddersfield

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 02.02.2019: Solskjaer, Hudson-Odoi, Willian, Bakayoko


Manchester United watampatia kazi meneja wao wa sasa Ole Gunnar Solskjaer akifanikiwa kushinda Paris St-Germain katika mchuano wao wa ligi ya mabingwa. (Sun)
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino ameelezea kutoridhishwa kwake na usimamizi wa klabu hiyo baada ya kushindwa kusajili wachezaji wapya kwa misimu miwili mfululizo. (Mirror    Chelsea watakabiliana na Bayern Munich katika uhamisho wa mshambuliaji Callum Hudson-Odoi, baada ya klabu hiyo ya Bundesliga kushindwa kumsajili nyota huyo wa miaka. (Sun)

Hudson-OdoiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionHudson-Odoi, wa kati

Winga Willian, 30 wa Chelsea na Brazil, anataka kusaini mkataba wa miaka mitatu, lakini kuna tetesi amepewa mkataba wa mwaka mmoja. (Sport Witness)
Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini alitaka kumsaini mchezaji wa zamani wa Cardiff, Gary Medel mwezi Januari lakini juhudi zake zilitibuka baada ya Besiktas kuitisha ada ya uhamisho. (Talksport)
Meneja wa Inter Milan Luciano Spalletti anaamini Arsenal "walimlaghai" winga wa Croatia Ivan Perisic, 29, katika pendekezo la uhamisho wa Januari. (Rai Sport via Independent)

Tiemoue BakayokoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTiemoue Bakayoko, kushoto

Kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 24, ambaye yuko AC Milan kwa mkopo kutoka Chelsea, amesema angependelea kusalia katika klabu huyo ya Italia. (Corriere dello Sport via Four Four Two)
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anahofia mlinzi wake Joe Gomez,21 huenda akahitaji kufanyiwa upasuaji. (Liverpool Echo)
Newcastle wanajianda kutangaza kuondoka kwa kocha wao wa zamani Peter Beardsley ambaye alikua mkufunzi wa timu ya wachezaji wa chini ya miaka -23. (Mail)

Mada zinazoh

Manchester United hawajashindwa hata mechi moja chini ya uongozi wa Ole Gunnar Solskjaer

Njombe: Mtoto mwengine apatikana msituni amefariki Tanzania

Mtoto mwengine alipatikana amefariki siku ya Ijumaa katika kijiji cha Matembwe wilayani Njombe huku visa vya vya mauaji kwa sababu ya matambiko na kutoweka kwa watoto vikiendelea kukumba eneo hilo.
Mwili wa mtoto huyo kulinga ana gazeti la The Citizen ulipatikana umetupwa katika msitu unaomilikiwa na wazazi wake mita chache kutoka nyumbani kwao.
Mwenyekiti wa kijiji cha Matembwe ameambia gazeti la The Citizen kwamba alipokea ripoti za mtoto huyo aliyepotea siku ya Ijumaa mwendo wa saa kumi na mbili jioni.Bwana Malekela alisema kuwa aliarifu jamii yote ambaypo ilianza kumsaka karibu na nyumbani kwao pamoja na msitu mbali na magari yaliokuwa katika eneo hilo.
Mamake mtoto huyo aliwasili kutoka kazini na kugundua kwamba mtoto wake alikuwa ametoweka.
Babake mtoto huyo bado alikuwa kazini wakati huo wote.
Kulingana na The Citizen Tanzania, mtoto aliyepatikana amefariki alikuwa ameenda shambani kulima na mamake, lakini baadaye mamake alimshauri kurudi nyumbani ili kufanya kazi nyengine
Lakini mama huyo alipowasili hakumpata mwanawe.
''Ni wakati huo ndiposa alimwambia mumewe na utafutaji ukaanza'' , alisema mwenyekiti wa kijiji hicho.
Ni hadi mwendo wa saa nne usiku ndipo mtoto huyo alipatikana amefariki akiwa na majeraha shingoni.
Mtoto huyo alizikwa hapo Jumamosi.
DC wa Njombe Ruth Msafiri alisema kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na wakati mgumu kutokana na misururu ya utekaji nyara watoto na mauaji.
''Serikali tayari imetuma jopo kuchunguza mauaji hayo na tayari jopo hilo limeanza kazi yake'', alisema katika mazishi siku ya Jumamosi Wilayani Njombe.

Waganga wa tiba ya Kienyeji


Baadhi ya Waganga wa tiba za jadi wilayani Njombe wakijadiliana jambo baada ya mkututano na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani

Kisa hicho kinajiri huku Waganga wa tiba za jadi wilayani Njombe nchini Tanzania wakijitenga na tuhuma kuwa wanachochea mauaji ya watoto wilayani humo.
Kwa mujibu wa serikali, uchunguzi wa awali umebaini kuwa mauaji ya watoto sita wilayani humo yamechochewa na imani za kishirikina.
Watoto hao, wakiwemo watatu wa familia moja wenye umri chini ya miaka 10 wamepatikana wakiwa wamefariki katika mazingira ya kutatanisha huku baadhi ya viungo vyao kama macho, meno na sehemu za siri vikinyofolewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola Jumatano aliliambia Bunge kuwa imani za kishirikina zimechochea matukio hayo na tayari serikali ina majina ya wahusika wote.
Hata hivyo, katika kikao chao na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni wilayani Njombe waganga wa jadi wamesema wao si chanzo cha tatizo na kuitaka serikali ifanye uchunguzi zaidi
Kiongozi wa waganga wa tiba za jadi Antony Mwandulami amedai kuwa watu wamekuwa wakilipiziana visasi kwa mauaji na kusingiziwa waganga wa jadi.
"Kuna mambo mengi nyuma ya haya mauaji. Wapo ambao wanalipiziana visasi na hawaonekani lakini waganga wanalaumiwa kwa kusemwa kuwa wamepiga ramli chonganishi," amesema Mwandulami.

Hofu yatanda


Waziri Masauni (katikati) akiogoza moja ya vikao wilayani Njombe kujadili mikasa hiyo ya mauaji ya watoto
Image captionWaziri Masauni (katikati) akiogoza moja ya vikao wilayani Njombe kujadili mikasa hiyo ya mauaji ya watoto

Mwandishi wa BBC Swahili Leonard Mubali anaripoti kutoka Njombe kuwa hofu imetanda wilayani hapo kutokana na matukio hayo ya mauaji.
Wazazi wameongeza uangalifu kwa watoto zao, na kuna ambao wanaacha shughuli zao na kusindikiza watoto shule.
Akizungumzia hofu hiyo waziri Masauni amesema: "Nachotaka kuwahakikishia wananchi ni kuwa macho, masikio, roho na moyo wa serikali umehamia Njombe. Waamini kuwa serikali jambo hili tumelichulia uzito mkubwa… ni jukumu letu kuwalinda wananchi ambao ndio wameiweka serikali hii madarakani. Lazima tuhakikishe kuna ulinzi, na hilo lipo ndani ya uwezo wetu na wala hatuna msalie mtume."
Akizungumzia kikao na waganga wa jadi Masauni amesema lengo lilikuwa ni kuunganisha nguvu na kupata taarifa zaidi kutoka kwao hususan kuwataja wale ambao wanachochea uovu.
Msafara wa mazishi ya watoto watatu wa familia moja waliokumbwa na mkasa huo.

US fake university: India anger after students arrested


University of Farmington fake website
Image captionThe sting operation came complete with a fake university website

India has made a diplomatic protest to the US after 129 Indian students were arrested for enrolling in a fake university.
The University of Farmington, advertised as based in Michigan state, was run by undercover agents from the Department of Homeland Security to expose "pay-to-stay" immigration fraud.
Prosecutors say those who enrolled knew that the facility would be illegal.
However, Indian officials say the students may have been duped.
On Saturday, the Indian Ministry of External Affairs (MEA) issued the protest to the US embassy in Delhi, expressing concern over the arrests and demanding consular access to those detained.
"Our concern over the dignity and wellbeing of the detained students and the need for immediate consular access for Indian officials to the detainees was reiterated," the ministry said.

How were students lured?

The fake university was set up in 2015 to try to catch foreign nationals who had initially travelled to the US on student visas and wanted to stay in the country, US media reported.
A website for the University of Farmington showed pictures of students in classes and libraries, or relaxing around a grassy campus.

University of Farmington fake website
Image captionThe website used stock images of students working

It advertised tuition for undergraduates at $8,500 (£6,500) a year and $11,000 a year for graduate students. It also had a fake Facebook page with a calendar of events.
But court papers released last week showed that the employees of the University of Farmington were undercover agents for the Immigration and Customs Enforcement agency (ICE).
The "campus" was an office at a business park in a Detroit suburb.

Who is being accused of what?

The indictment, filed in the District Court for the Eastern District of Michigan, said the students knew the scheme was illegal.
Prosecutors say the spurious university was being used as a "pay to stay" scheme - allowing people who entered the country legally as students to extend their stay and work by transferring to it.
A total of 130 students - including 129 from India - were arrested on Wednesday and charged with civil immigration charges, the Detroit Free Press reported.
The students face possible deportation if convicted.
Separately, eight people who allegedly acted as recruiters were charged with conspiracy to commit visa fraud and "harbouring aliens for profit".

What is India arguing?

The Indian government said the students could have been tricked into enrolling.
"We have urged the US side to share full details and regular updates of the students with the government, to release them from detention at the earliest and not to resort to deportation against their will," MEA added.
Some immigration advocates in the US also believe innocent foreigners were trapped by the government.
Ravi Mannam, an immigration attorney in Atlanta, told the Detroit Free Press that the sting "kind of hooked these students by promising them credits for their previous master's programmes".
Meanwhile a telephone hotline for worried relatives of those being held has been set up at the Indian embassy in Washington, the Times of India reported.
The US embassy in Delhi confirmed it had received the note of protest but made no further statement.

What is behind the crackdown?

US immigration authorities have resorted to increasingly tough enforcement tactics in recent years.
In a precedent to the latest sting, immigration agents set up the fake University of Northern New Jersey in 2016 under the Obama administration. A total of 21 people, mostly from China and India, were arrested.
Over the past two years, the Trump administration has further clamped down on undocumented migrants and visa overstayers.
Workplace raids have led to hundreds of arrests.
In two massive operations last year, ICE agents detained 146 people at a meat supplier in Ohio and another 150 at a trailer manufacturer in Texas.



Media captionThe missing - consequences of Trump's immigration crackdown

Related Topics

University of Farmington fake website